Star Tv

Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli amemuagiza waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Suleiman Jaffo kumfukuza kazi mtumishi wa halmashauri ya wilaya ya kilosa Daniel Elimringi kwa kosa la kuchana kitabu kitakatifu cha dini ya kiislam,qur’ani.

Taarifa na Piensia Rugarabamu

Rais Magufuli ametoa agizo hilo wakati akizungumza na wakazi wa Kigamboni mara baada ya kuzindua wilaya mpya ya kigamboni iliyoambatana na uzinduzi wa jengo la utawala la mkuu wa wilaya hiyo ambapo amesema licha ya Waziri Jafo kumsimamisha kazi mtumishi huyo, serikali haiwezi kufanya kazi na watumishi wa namna hiyo.

Katika hatua nyingine rais Magufuli ameiagiza Wizara ya Ardhi kuhakikisha zaidi ya hekari 750 za ardhi iliyokuwa shamba la nafco napco zilizoko chini ya wizara ya ardhi zinarejeshwa kwa manispaa ya Kigamboni ndani ya wiki mbili.

Akifafanua kuhusu jengo hilo mkuu wa wilaya ya kigamboni Sarah Msafiri amesema litasaidia wakazi wa wilaya hiyo kupata huduma kwa urahisi huku akibainisha kupungua kwa matukio ya uhalifu katika wilaya hiyo na kuhaidi kumalizika kwa utekelezwaji wa mradi wa umeme hivi karibuni.

Viongozi mbalimbali waliohudhuria uzinduzi huo wamebainisha changamoto zilizopo katika wilaya hiyo.

Hata hivyo Rais Magufuli ameendelea kutoa onyo kwa wananchi wanaoishi mabondeni konte nchini kuzingatia agizo la waziri mkuu kuondoka maeneo hayo na kwamba serikali haitojihusisha kugharamia athari za mafuriko kwa wote wanaokaidi agizo hilo.

                                                                     Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.