Star Tv

Serikali inaendelea kuchunguza kwa kina uwepo wa tishio la uvamizi  wa  Nzige  ambao wanadaiwa kuingia katika maeneo ya  Mwanga na Holili mkoani Kilimanjaro mpakani mwa Tanzania na Kenya.

Taarifa na Zephania Renatus

Taarifa  zilizozagaa  kwenye mitandao ya kijamii na ambazo zimezua taharuki kwa watanzania ni  juu ya tishio la uvamizi wa  Nzige  ambao wanadaiwa kuingia katika badhi ya maeneo ya Wilaya ya  Mwanga karibu na nchi jirani ya Kenya.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt.Anna Mghwira amezungumza na waandishi wa habari  na na kuwatoa wasiwasi watanzania kuwa nzige hao huenda walipita tu katika baadhi ya maeneo ya Mkoa huo.

Taarifa hiyo inakuja huku baadhi ya wakazi wa maeneo ya Holili na Taveta  katika Mpaka wa Tanzania na Kenya  hawajaona nzige hao na bado wanaonekana katika baadhi ya maeneo ya nchi jirani ya Kenya.

Wakati hofu hiyo ikiendelea kutanda ,hata hivyo wakulima katika maeneo ya mpakan wanaomba serikali kuchukua tahadhari  kabla wadudu hao hawaingia nchini Tanzania.

                                                                       Mwisho

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.