Star Tv

Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour Party TLP Augustino Mrema ameitaka Serikali kumlipa Shilingi bilioni mbili kama fidia ya kesi alizowahi kushtakiwa chini ya serikali ya awamu ya tatu iliyokuwa inaongozwa na Rais mstaafu Benjamin Mkapa.

Mrema ametoa kauli hiyo katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini dar es salaam wakati akizungumzia hali ya kisiasa nchini katika kipindi cha miaka 24 iliyopita hadi sasa.

Mwenyekiti huyo wa TLP amesema kutokana na misukosuko aliyoipata kwa kufunguliwa kesi za mara kwa mara, Serikali inapaswa kumlipa fidia ya kiasi hicho cha fedha.

 “Ninataka serikali ya CCM ambayo ndio imenufaika na mateso niliyopata kwa miaka yote wanifidie shilingi bilioni 2, hela ndogo ya chumvi na wasiponifidia nitawashtaki kwa watanzania.” Amesema Augustino Mrema-Mwenyekiti wa TLP Taifa.

Katika hatua nyingine Mrema amesema hakufurahishwa na vitendo vilivyofanywa katika uchaguzi wa serikali za mitaa hasa katika kijiji cha Kiraracha wilayani Moshi Mkoani Kilimanjaro akieleza kuwa zilikuwa ni hujuma za wazi dhidi yake.

Mbali na fidia, pia Mrema aliyepata kugombea nafasi ya Urais na kuleta upinzani mkubwa katika uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi wa mwaka 1995 amemuandikia barua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli iliyo na malalamiko na kuomba kukutana naye ili waweze kuzungumza.

                                                                                                       Mwisho.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.