Star Tv

Jamii za makabila yanayojihusisha na vitendo vya ukeketaji mkoani Manyara zimesema ili ziondokane na mila hiyo ni vema zikapewa elimu kwa njia mbalimbali itakayosaidia kubadili fikra  kuwa, vitendo hivyo  vinafaida kwa mwanamke.

Wanajamii hao wamesema wanapaswa kupewa elimu ya kina kwa njia mbalimbali zitakazowabadilisha fikra ili  kuachana na mila hiyo potofu.Baadhi ya makabila yanayojihusisha na ukeketaji mkoani Manyara ni wamasai, wairaq,wanyaturu au watatoga na wabarbaig.

Kwa upande wao viongozi wa madhehebu ya dini wanaopinga ukeketaji huo wanaona ukatili huu kwa mwanamke haufai hivyo ni vyema sheria za haki za  binadamu  zikasimamiwa ipasavyo.

Shirika la CSP linalojihusihsa na shughuli za kupinga ukatili kwa jamii limeanza harakati za kutokomeza vitendo hivyo mkoani Manyara  kwa njia mbalimbali ikiwemo kuwaelimisha vijana wadogo.

Takwimu za mwaka 2016 zinaonyesha kuwa, mkoa wa Manyara unaongoza kwa ukeketaji kwa asilimia 58.8, ukifuatiwa na mkoa wa Dodoma asilimia 47, mkoa wa Tatu ni  Arusha asilimia 41,Mara asilimia 32,Singida asilimia 31 Tanga asilimia 14 na Kilimanjaro asilimia 10.

                                                                                             Mwisho.

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.