Star Tv

Wakati Jumuiya ya Afrika mashariki inaadhimisha miaka ishirini tangu kuanzishwa kwake.  inaelezwa nusu ya wakazi wa nchi wanachama wa jumuiya hiyo bado ni maskini wanaoishi kwa kutegemea misaada kutoka nje .

Pamoja na hali hiyo, inaelezwa kuwa kuna mafanikio yaliyopatikana miongoni mwa nchi wanachama, ingawa jitihada zinahitajika zaidi katika kuboresha hali ya uchumi wa nchi moja moja, kama anavyoeleza Katibu mkuu wa jumuiya hiyo Liberart Mfumukeko.

Miongoni mwa mafanikio yanayotajwa, ni pamoja na matumizi ya lugha ya Kiswahili, licha ya kuwepo kwa mkanganyiko iwapo lugha hiyo iwe rasmi ndani ya Jumuiya au la.

 Pamoja na changamoto za hapa na pale zinazoikabili jumiya hiyo, likiwemo suala la ulipaji wa ada za kila mwaka kwa nchi wanachama, sekretarieti ya jumuiya hiyo inajivunia mafanikio yaliyopatiakan hadi sasa. Injinia Steven Mlote ni Naibu katibu mkuu wa Jumuiya hiyo.

 Kilele cha maadhimisho ya miaka 20 tangu kuanzishwa kwa jumuiya ya Afrikla mashariki, itakuwa Novemba 30 mwaka huu.

 

                                                    

                                                          Mwisho

 

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.