Star Tv

Mkoa wa Simiyu umezindua mkakakati wa kuboresha taaluma kwa mwaka 2020 ili kuinua taaluma katika maeneo yote.

Afisa Elimu Mkoa wa Simiyu, Ernest Hinju, amesema mkakati huo wa kitaaluma kwa mwaka 2020, unawaelekeza viongozi hasa wa sekta ya elimu kutumia uwezo wao kufikiri, kubuni na kuhakikisha mikakati waliyojiwekea inafanikiwa.

Akizindua mkakati huo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini, amesema walimu wanayo kazi moja tu ya kutibu adui ujinga, na kwamba maadui wengine ambao ni maradhi na umasikini yatatoweka wapo watu wataelimika.

Pamoja na maafisa elimu wilaya na kata, watekelezaji wakuu wa mpango huu ni walimu wakuu na wakuu wa shule ambao licha ya changamoto zilizopo wameahidi mafanikio.

Mkakati huo pia unalenga kushirikisha kada zote, ikiwemo viongozi wa kisiasa na jamii ili kufikia mafanikio ya kitaaluma.

                                                                     Mwisho

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.