Star Tv

Mfanyabiashara wa vyuma chakavu wilayani Serengeti mkoani Mara imembidi kujisalimisha kwa jeshi la polisi mjini humo baada ya kugundua kauziwa Bomu kwa shilling elfu nne kama chuma chakavu.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida mfanyabiashara wa vyuma chakavu mjini Mugumu wilayani Serengeti mkoani Mara Jonas Marwa amejikuta katika wakati mgumu baada ya kugundua kauziwa Bomu kama chuma chakavu kwa shilling elfu nne. Baada ya kubaini kitu hicho kinacho shabihiana na bomu ndipo alipokwenda polisi kuomba msaada. Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huu imefika na kushuhudia bomu hilo huku wakikiagiza kikosi cha jeshi la wananchi wa Tanzania 21 KJ kufika na kulitegua. Ununuzi wa vyuma chakavu katika maeneo mengi mkoani Mara ni moja ya vitu vinachotakiwa kuwekewa utaratibu maalumu kutokana na wanunuzi na waletaji wa bidhaa chakavu kutokuwa makini na kuokota vitu vinavyoweza kuleta madhara katika jamii.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.