Mfanyabiashara wa vyuma chakavu wilayani Serengeti mkoani Mara imembidi kujisalimisha kwa jeshi la polisi mjini humo baada ya kugundua kauziwa Bomu kwa shilling elfu nne kama chuma chakavu.
Katika hali isiyokuwa ya kawaida mfanyabiashara wa vyuma chakavu mjini Mugumu wilayani Serengeti mkoani Mara Jonas Marwa amejikuta katika wakati mgumu baada ya kugundua kauziwa Bomu kama chuma chakavu kwa shilling elfu nne. Baada ya kubaini kitu hicho kinacho shabihiana na bomu ndipo alipokwenda polisi kuomba msaada. Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huu imefika na kushuhudia bomu hilo huku wakikiagiza kikosi cha jeshi la wananchi wa Tanzania 21 KJ kufika na kulitegua. Ununuzi wa vyuma chakavu katika maeneo mengi mkoani Mara ni moja ya vitu vinachotakiwa kuwekewa utaratibu maalumu kutokana na wanunuzi na waletaji wa bidhaa chakavu kutokuwa makini na kuokota vitu vinavyoweza kuleta madhara katika jamii.