Star Tv
KUKITHIRI kwa tabia ya ulevi wakupindukia kwa baadhi ya wazazi na walevi mjini Iringa, kumetajwa kuathiri kundi la watoto na kusababisha idadi kubwa ya watoto kuishi katika mazingira hatarishi, baada ya wazazi wao kutozingatia mahitaji ya familia zao.
 
Ulanzi ni miongoni mwa pombe za jadi zinazopatikana mkoani Iringa - pombe inayogemwa kuanzia mwezi wa pili mpaka mwezi wa tano, ingawa zipo pombe nyingine nyingi za jadi kama Komoni  pombe inayopikwa kwa kutumia Mahindi na Ulezi, huku nayo pombe aina ya Msabe na Kimpumu zikipatikana kwa wingi mkoani Iringa, ambapo Mwenyekiti wa wenyeviti wa Kata 
 
ya Ruaha-Timoth Kiongozi, anasema tatizo la ulevi wa pombe kwa baadhi ya wazazi na walezi ni kubwa. Zainabu Mgimbe ni miongoni mwa viongozi wa Kata ya Ruaha, anasema katika sensa waliyoifanya katika Kata hiyo ya Ruaha, wamebaini uwepo wa idadi kubwa ya watoto waishio katika mazingira hatarishi ambao baadhi yao ni yatima na wengine wazazi na walezi wao ni walevi.  Baadhi ya watotot wanakosa malezi bora kutokana na walezi/wazazi kuwa walevi.
 
 
 
 
 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.