Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Bw. Adolf Hyasinth Mohondela Ndunguru kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango anayeshughulikia Sera.
Bw. Ndunguru ameteuliwa kushika nafasi ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango (Sera) ambayo ilikuwa wazi.
Kabla ya uteuzi huo Bw. Ndunguru alikuwa Naibu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Kufuatia Uteuzi huo, Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. Msafiri Lameck Mbibo kuwa Naibu Kamishna Mkuu wa TRA.
Kabla ya Uteuzi huo Bw. Mbibo alikuwa Meneja wa TRA Mkoa wa Kilimanjaro.
Uteuzi wa viongozi hao unaanza mara moja leo tarehe 31 Machi, 2019.
Chanzo: Ikulu Dar es Salaam.