Hatimaye Wananchi wa Kijiji cha nyakafuro wakubali kuupokea Mwili wa Marehemu Jackson Charles anayedaiwa kusababishiwa kifo kutokana na kipigo cha polisi baada ya Mkuu wa Wilaya ya Geita Josephat Maganga kuingilia kati mgogoro huo na kuwaahidi kufanya uchunguzi wa jambo hilo na kama kuna makosa hatua za kisheria zitachukuliwa.
Machi 24 nido alifariki Marehemu Jackson na Wananchi wakagoma kuzika ambapo mwili ulihifadhiwa Hospitali teule ya Mkoa wa Geita.
Wanakijiji hawa wanaamini kipigo ndio kimesababisha kifo lakini taarifa ya Polisi imeeleza kuwa arehemu alikua na kifafa na Malaria.
Wananchi wanabainisha kuwa ushirikiano wa polisi na Wananchi haupo na kutaka polisi waliokuwepo kubadilishwa.
Wananchi wanaridhia kuzika ambapo Mkuu wa Wilaya ya Geita josephat Maganga ameagiza uongozi wa Wilaya kutoa ardhi ambapo Serikali ya kijiji imeridhai kwa hilo kwani familia haina eneo na walikua wamepanga tu.
Siku mbili za uchunguzi zimetolewa na ikibainika ukiukwaji umefanyika hatua stahiki zitachukuliwa baada ya kujiridhisha pa kuwa na mashaka.