Star Tv

Spika wa bunge la jamuhuri ya Tanzania ndugu, Job Ndugai amewataka watanzania kuonesha uzalendo kwa kutumia ndege za shirika la ndege la Tanzania kuonesha uzalendo na kujivunia kodi yao iliyonunua ndege hizo kwa Mataifa mengine.

 

Kauli hiyo ameitoa  jijini dodoma wakati akihutubia ufunguzi wa ofisi mpya za shirika hilo mjini dodoma. Akizungumza kwenye uzinduzi ndugu Job Ndugai amesema kuwa watanzania wanapaswa kuonesha uzalendo wa hali ya juu kwa shirika lao la ndege kwani raia wa mataifa mengine yenye mashirika ya ndege huthamini ndege za mashirika yao.

 Sambamba na hilo amewataka wasimamizi wa shirika hilo kuhakikisha shirika  halididimii bali liimarike zaidi. Kwa upande wake waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano Isaack Kamwelwe amewatoa shaka watanzania juu ya usalama wa ndege akiwataka kutoogopa kwani kuna usimamizi madhubuti ndani na makapuni yanayotengeza ndege nakutoa pole kwa ajali zilizotokea

 Mkurugezi mkuu wa shirika la ndege ATCL amesema kuwa ipo mikakati kadhaa kuhakiksha ndege zinafika maeneo mbalimbali na tayari wameanza safari kwenye maeneo mengine.

 

Mbali na kufunguliwa tawi hilo shirika la ndege la ATCL limekuwa likifanya safari zake kutoka sehemu mbalimbali na kutua Dodoma kwa muda sasa.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.