Star Tv

 

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Mheshimiwa Kassim Majaliwa ameziagiza taasisi za fedha chini ya Benki kuu ya Tanzania kuanzisha  kitengo maalum ndani ya taasisi hizo kitakachokuwa kinapokea madini ya dhahabu kama dhamana ya mkopo kwa wachimbaji wa madini ikiwa ni sambamba na kuangalia namna ya kupunguza riba ili iwe nafuu kwa wachimbaji wadogo.

 

Amezungumza haya wakati wa kufunga maonyesho ya teknolojia ya dhahabu Mjini Geita. Waziri alianza kutembelea baadhi ya mabanda yakiwemo ya kifedha na kuona namna gani wanavyotoa kipaumbele katika mikopo kwa wachimbaji wadogo.

 Katika maonyesho haya ambayo kila sekta inayohusiana na madini iliweza kutoa elimu kama banda la kliniki ya biashara na banda la waja linalosisitiza utumiaji sahihi wa kemikali za dhahabu.

 

 Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel amesema dhahabu ya Geita sasa inatakiwa iakisi maisha ya Wanageita kwa kupata huduma bora na wale wote waliotumia  fedha  za jamii zinazotolewa na mgodi watachukuliwa hatua.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.