Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Mheshimiwa Kassim Majaliwa ameziagiza taasisi za fedha chini ya Benki kuu ya Tanzania kuanzisha kitengo maalum ndani ya taasisi hizo kitakachokuwa kinapokea madini ya dhahabu kama dhamana ya mkopo kwa wachimbaji wa madini ikiwa ni sambamba na kuangalia namna ya kupunguza riba ili iwe nafuu kwa wachimbaji wadogo.
Amezungumza haya wakati wa kufunga maonyesho ya teknolojia ya dhahabu Mjini Geita. Waziri alianza kutembelea baadhi ya mabanda yakiwemo ya kifedha na kuona namna gani wanavyotoa kipaumbele katika mikopo kwa wachimbaji wadogo.
Katika maonyesho haya ambayo kila sekta inayohusiana na madini iliweza kutoa elimu kama banda la kliniki ya biashara na banda la waja linalosisitiza utumiaji sahihi wa kemikali za dhahabu.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel amesema dhahabu ya Geita sasa inatakiwa iakisi maisha ya Wanageita kwa kupata huduma bora na wale wote waliotumia fedha za jamii zinazotolewa na mgodi watachukuliwa hatua.