Star Tv

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein leo amefanya uteuzi wa viongozi katika Taasisi mbali mbali za Serikali ya Mapinduzi.

 

Kwa mujibu wa Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, Rais Dk. Shein amemteua Dk. Abdulla Mohamed Juma kuwa Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii ambaye anachukua nafasi ya Dk. Vuai Idd Lila ambaye atapangiwa kazi nyengine.

 

Katika uteuzi huo pia, Rais Dk. Shein amemteua Khalfan Sheikh Saleh kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Serikali wa Uchapaji na Mpigachapa Mkuu wa Serikali, ambaye anachukua nafasi ya Mohamed Suleiman Khatib ambaye atapangiwa kazi nyengine.

 

Aidha, Rais Dk. Shein amemteua Said Juma Ahmada kuwa Mkurugenzi wa Baraza la Manispaa ya Mjini Unguja, Mkurugenzi huyo wa Manipaa ya Mjini Unguja anachukua nafasi ya Aboud Hassan Serenge ambaye anastaafu kwa mujibu wa Sheria.

 

Pia, Rais Dk. Shein amemteua Amour Ali Mussa kuwa Mkurugenzi wa Baraza la Manispaa ya Magharibi “A”, Amour Ali Mussa anachukua nafasi ya Said Juma Ahmada ambaye amehamishiwa Manispaa ya Mjini.

 

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.