Soko maarufu la mitumba jijini Mwanza lawaka moto na kukusanya umati wa watu wakishuhudia vitu vikiungua.
Soko hili maarufu kwa kuuza mitumba jijini Mwanza limewaka moto leo. Akiongea Mwenyekiti wa soko hilo ndugu Mansoor Ahmed ameiambia Star TV Habari kuwa moto huo ulianza majira ya alfajiri na ambapo chanzo cha moto bado hakijajulikana, huku mali zilizoteketea mpaka sasa thamani yake hazijajulikana pia.
Nae kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Jonathan Shana, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku wananchi na jeshi la polisi wakishirikiana kuudhibiti ili usilete madhara zaidi.