Waziri mkuu wa Tanzania Kasim Majaliwa amewata Wanajumuiya ya WANAJIOSAYANSI kuwa wa kwanza kujua kinachoendelea katika sekta zote zinazowahusu bila kujali wanafanya kazi serikalini au Shirika Binafsi kwa maslahi mapana ya Taifa.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametoa kauli hiyo Jijini Dodoma wakati akifungua warsha ya wana jumuiya hiyo ambapo Sekta ya Madini, Maji na mafuta ni kati ya sekta zinazowahusu wanajioSayansi.
Waziri wa Madini Angellah Jasmin Kairuki akitoa ufafanuzi amesema, "sekta ya madini inafulsa kubwa ili kuongeza ufanisi na uwezo wa kiuchumi wa wanajiosayansi".
Kwa upande wake Dk, Elisante Mshiu katibu mkuu wa wanajiosayansi Tanzania anasema lengo la kuanzishwa kwa jumuiya hiyo ni kuleta wanasayansi ili kujadili Sayansi ya dunia na Mifumo yake.
Katika kuhakikisha Sekta ya madini inaleta matokeo chanya hapa nchini serikali iliifanyia marekebisho ya sheria ya madini ya mwaka 2010 ili sekta ya madini iweze kumilikiwa na wazawa kwa sehemu kubwa.