Kivuko cha MV Kitunda kinachofanya safari zake kutoka Lindi mjini Kuelekea ng’ambo ya pili ya bahari kimesitisha safari zake baada ya kupata hitilafu za kiufundi
Kutokana na kivuko hiki kusitisha safari zake hali hiyo imewalazimu wakazi wa kata ya Kitumbikweal mkoani Lindi kukosa huduma ya usafiri huku baadhi yao wakilazimika kutumia mitumbwi.
Mapema leo hii Halmashauri ya manispaa waliombwa boti yake ianze kutoa huduma pamoja na mitumbwi ya watu binafsi ambayo ni salama kwa usafirishaji.