Star Tv

Wabunge nchini Tanzania watapimwa virusi vya HIV siku ya Alhamisi ikiwa ni mfano wa kuwa katika mstari wa wa mbele katika jitihada za kupambana na ugonjwa wa ukimwi, kwa mujibu wa gazeti la Citizen la nchini humo.

Mwenyekiti wa kamati ya bunge inayohusika na masuala ya HIV, Bw Oscar Mukasa, alisema Jumanne kuwa kundi hilo litaandaa shughuli kadhaa kuunga mkono kampeni ya serikali ya nchi nzima ya kupima virusi vya HIV, wakati wa kampeni iliyozinduliwa na waziri mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa siku ya Jumanne.

Kampeni hiyo inayofahamika kama 'Furaha Yangu' inafanywa kwa ushirikiano kati ya serikali ya Tanzania na shirika la maendeleo ya kimataifa la Marekani la USAID, mradi ya afya wa Tugole na washikadau wengie katika sekta ya afya.

Kati ya shughuli zingine ambazo zitachukuliwa na bunge kwa mujibu wa Bw Mukasa ni pamoja na kongamano kuhusu wajibu wa viongozi katika kupambana na virusi vya ukimwi.

Pia kutakuwa na maonyesho kuhusu shughuli zinazofanywa na mashirika yasiyo ya serikali katika kupambana na virusi vya ukimwi kuanzia Ijumaa hadi Jumamosi.

Kwa hisani ya BBC.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.