Star Tv

Mkurugenzi Mkuu Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu amesema hali ya upatikanaji wa dawa nchini Tanzania imeimarika hadi kufikia asilimia 90. Akizungumza na waandishi wa habari, Bwanakunu amesema kuna upatikanaji wa dawa muhimu takribani 135.

“Upatikanaji wa dawa hizi muhimu kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ni kati ya asilimia 85 hadi 98, ambapo dawa za kupunguza makali ya virusi vya Ukimwi na malaria ni asilimia 100,” -Bwanakunu Pia Bwanakunu amesema MSD imetunukiwa Ithibati ya Kimataifa ya Juu ya Ubora inayojulikana kama ISO 90001:2015 ambayo itadumu kwa miaka 3. “Kampuni ya Kimataifa ya ACM Ltd ilifanya ukaguzi wa ubora wa huduma zinazotolewa na MSD August 2017, ambapo matokea yalithibitisha kuwa huduma tunazotoa za ununuzi, utunzaji na usambazaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara zinafuata miongozo ya Kimataifa,”-Bwanakunu Mbali na hilo, pia amebainisha kuwa wameanzisha mfuko wenye vifaa vya kujifungulia wakina mama ambao utakuwa na vifaa vyote na utauzwa Shilingi Elfu Kumi na Mbili.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.