Star Tv

Uongozi wa Shule ya Sekondari ya Tabora Wasichana umeipongeza serikali kwa hatua yake ya kuziondoa kaya zaidi ya 60 zilizokuwa zimejenga katika eneo la shule hiyo ili kuimarisha usalama wa wanafunzi na mali zao.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Tabora Wasichana Mwl. Lydia Eliud, amesema sehemu kubwa ya shule hiyo ilivamiwa na wakazi wa Kata ya Ng’ambo hivyo kuhatarisha maisha ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu na wizi kwenye mabweni nyakati za usiku. Mkuu wa Shule ya Tabora Wavulana Mwl. Robert Marwa ameelezea ufaulu mzuri wa mwanafuzi wake Clarence Sumbuzi aliyekuwa wa 8 kitaifa kwa masomo ya Sayansi huku Agatta Nyenga aliyekuwa wa 2 kati ya Mwanafunzi 10 wa Kitaifa kutoka Shule ya Sekondari ya Tabora Wasichana .

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tabora ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mwl. Queen Mlozi amewataka walimu wakuu wa shule zote za Sekondari kuhakikisha wanasimamia nidhamu za wanafunzi.

Katika kikao hiki cha kazi cha wakuu wa shule za sekondari za mkoa huu wametakiwa kuchukua hatua dhidi ya wanafunzi ambao hawana nidhamu kwenye shule zao mapema ili wasiweze kusababisha vijana wengine ambao ni wazuri nao wakaiga tabia zao.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.