Star Tv
Ndoto na Shauku ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda kuweka Mazingira Bora ya Walimu inakaribia kutimia ambapo leo amefanya Uzinduzi wa Zoezi la Kuezeka Mabati kwenye ujenzi wa Ofisi 402 za Walimu Dar es salaam na kupokea hundi ya Shilingi Million 50 kutoka kampuni ya mawasiliano ya Halotel iliyoguswa na kampeni ya Ujenzi wa Ofisi za Walimu Dar. Ujenzi wa Ofisi hizo 402 ni jitiada za RC Makonda kuboresha Mazingira ya Walimu baada ya kufanya kikao na Wakuu wa Shule na kugundua walimu wanafanya kazi katika Mazingira Magumu ikiwemo kufanya kazi zao Chini ya Miti na ukosefu wa Vyoo. Kama ilivyo kawaida yake kutoa Majibu kwenye changamoto RC Makonda aliamua kuanza kampeni ya Ujenzi wa Ofisi 402 za walimu Dar es salaam zenye hadhi ambapo ndani yake kuna Ofisi ya Mwalimu Mkuu, Mwalimu Mkuu Msaidizi, Ofisi ya Walimu wote, Vyoo, Bafu, Jiko, Ofisi ya Mhasibu, Chumba cha kuhifadhi Nyaraka, Chumba cha kubadilisha Nguo, Mapokezi, Ukumbi wa Mkutano na vifaa vya kisasa kutoka Marekani ikiwemo Meza, Viti, Computer, AC na TV. RC Makonda amesema ndoto na shauku yake ni kuona Elimu Bora inatolewa ili kusaidia Taifa kuwa na Wataalamu wa kutosha kuepuka kuchukuwa Wataalamu kutoka Nje ya Nchi na ili kufikia huko ni lazima Walimu wawekewe Mazingira Bora ya kufanya kazi kwakuwa tayari Rais Magufuli ameshaonyesha Dira kwa kutoa Elimu Bure ili kumwezesha Mtoto wa Maskini kuwa na utajiri na kunufaika na rasilimali za Nchi hii. Aidha Makonda ameishukuru kampuni ya Mawasiliano ya Halotel kwa kuchangia kiasi cha Shilingi Million 50 kama sehemu ya awamu ya kwanzaa ambapo wameahidi kuongeza Million 50 nyingine. RC Makonda amesema katika awamu ya kwanza watakabidhi Ofisi 100 na kuwaomba Wananchi kushirikiana na Serikali kwa kuendelea kuchangia kampeni hiyo ili kuwawezesha Walimu kufanya kazi katika mazingira mazuri. Nao baadhi ya Walimu walioshiriki uzinduzi huo wamemshukuru RC Makonda kwa kuwajengea ofisi hizo zenye hadhi ya kipekee ambazo zinaenda kumaliza changamoto ya muda mrefu kufanya kazi chini ya miti,madarasani pamoja na ukosefu wa vyoo. Pia Walimu hao Wamemshukuru RC Makonda kwa kuwawezesha kusafiri Bure kwenye usafiri wa Umma na kupata Viwanja vya Bei nafuu. TUSHIRIKIANE KWA PAMOJA KUWEKA MAZINGIRA BORA YA ELIMU DAR ES SALAAM

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.