Star Tv

Halmashauri ya wilaya ya Serengeti mkoani Mara imeshindwa kufikia lengo la kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 44 na milioni 236 za kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kipindi cha mwaka 2016 - 2017.

Halmashauri ya wilaya ya Serengeti iliyopo mkoani Mara, uwenda ikashindwa kufikia malengo yake ya kuwapatia huduma bora wakazi wa wilaya hiyo kufuatia kushindwa kukusanya kiasi cha shilling billion 44,236,729,524 na kuambulia mapato ya shilling billion 3,185,575,982 sawa na asilimia 10 tu ya makusanyo yote ya ndani.

Wakizungumza katika mkutano wa hadhara na wananchi wilyani humu, viongozi wa halimashauri hiyo, wamesema kuwa upungufu huo unatokana na dosali zitokanazo na watendaji kutokusimamia vema mapato.

Wakizungumzia huduma mbali mbali viongozi hawa wanasema kuwa serikali ya awamu ya tano ipo makini kuhakikisha inawaletea maendeleo wananchi wake. Halmashauri ya wilaya ya Serengeti ni kati ya halmashauri nane zilizopo mkoani Mara,pamoja na uwepo wa hifadhi ya taifa ya Serengeti katika wilaya hii bado inakabiliwa na tatizo la kushindwa kukusanya mapato yatokanayo na tozo la huduma katika mahotel ya kitalii.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.