Halmashauri ya wilaya ya Serengeti mkoani Mara imeshindwa kufikia lengo la kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 44 na milioni 236 za kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kipindi cha mwaka 2016 - 2017.
Halmashauri ya wilaya ya Serengeti iliyopo mkoani Mara, uwenda ikashindwa kufikia malengo yake ya kuwapatia huduma bora wakazi wa wilaya hiyo kufuatia kushindwa kukusanya kiasi cha shilling billion 44,236,729,524 na kuambulia mapato ya shilling billion 3,185,575,982 sawa na asilimia 10 tu ya makusanyo yote ya ndani.
Wakizungumza katika mkutano wa hadhara na wananchi wilyani humu, viongozi wa halimashauri hiyo, wamesema kuwa upungufu huo unatokana na dosali zitokanazo na watendaji kutokusimamia vema mapato.
Wakizungumzia huduma mbali mbali viongozi hawa wanasema kuwa serikali ya awamu ya tano ipo makini kuhakikisha inawaletea maendeleo wananchi wake. Halmashauri ya wilaya ya Serengeti ni kati ya halmashauri nane zilizopo mkoani Mara,pamoja na uwepo wa hifadhi ya taifa ya Serengeti katika wilaya hii bado inakabiliwa na tatizo la kushindwa kukusanya mapato yatokanayo na tozo la huduma katika mahotel ya kitalii.