Star Tv

Waziri wa Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ameiomba Taasisi ya Africa Academy for Public Health kushirikiana na Serikali kufanya tafiti zenye tija kwenye magonjwa kama TB na Ukimwi ili kupunguza changamoto ya magonjwa hayo nchini.

Waziri Ummy ametoa kauli hiyo katika uzinduzi wa mpango mkakati wa miaka mitatu kuanzia mwaka 2018 hadi 2020 wa taasisi Africa Academy for Public Health Jijini Dar Es Salaam. Mkakati huo ua lengo la kukuza tafiti za mfumo wa afya, ubunifu na matumizi ya takwimu katika kuboresha ustawi wa watu.

Dhima ya Taasisi ya ya Africa Academy for Public Health ni pamoja na kushirikiana na Serikali, wadau wa afya katika tafiti mbali mbali za afya hususani zinazohusu afya ya mama na watoto masuala ya lishe, magonjwa yasiyo ya kuambukiza na yale ya kuambukiza.

Picha na mtandao.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.