Star Tv

Serikali imewatoa wasiwasi wakulima wa Pamba mkoani Morogoro juu ya upatikanaji wa soko pamoja na pembejeo ambapo mnunuzi atakayenunua Pamba yote itakayozalishwa amepatikana.

Akizungumza na wakulima wa zao hilo katika kijiji cha Makuyu wilayani Mvomero mkoani hapa, mkuu wa mkoa wa Morogoro Dr.Kebwe Stephen, amesema historia inaonyesha mkoa wa Morogoro ndio mwasisi wa kilimo cha zao la Pamba, na lilikuwa tegemeo kubwa la kiuchumi kwa wakulima na Serikali ya mkoa.

Dr Kebwe amesema serikali inatambua changamoto zilizopelekea baadhi ya wakulima kuamua kuachana na kilimo cha zao hilo, hususani kukosekana kwa soko la uhakika, jambo ambalo limeshapatiwa ufumbuzi.

Marco Mtunga ni mkurugenzi wa bodi ya Pamba nchini ,amesema wakulima wa zao la pamba wana fursa kubwa kupiga hatua kiuchumi ikilinganishwa na mazao mengine ya biashara, hivyo kuwataka kuwatumia wataalamu wa kilimo katika maeneo yao, na kufanya kilimo chenye tija.

Na hapa baadhi ya wakulima wa zao la pamba wilayani Mvomero,wakabainisha changamoto mbalimbali zilizokwamisha kilimo cha zao hilo.

Pamba ni kati ya mazao matano ya biashara yaliyopewa kipaumbele na serikali ya wamu ya tano kutaka kufanikisha adhma ya serikali ya viwanda na nchi ya uchumi wa kati ifikapo 2025 ambapo makisio kwa wilaya ya Mvomero pekee ni kufikia wastani wa tani 293 za mavumo kwa msimu wa kilimo 2017/2018 huku wakulima zaidi ya 290 wamehamasika kujikita katika kilimo hicho.

Picha na mtandao.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.