Star Tv

Wizara ya mambo ya ndani kupitia idara ya uhamiaji mkoani Mtwara kwa kushirikiana na Jeshi la Wananchi (JWTZ) imewakamata wahamiaji 67 wasiofata sheria na wenye uraia wa nchini Ethiopia.

Raia hao ambao walikua walielekea nchini Msumbiji kwa njia ya bahari waliongozwa na mtanzania kutoka visiwa vya Pemba ajulikanae kwa jina la Bakari Ally.

Wahamiaji hao walikuwa wakitoka Mombasa nchini Kenya wakielekea nchini Afrika Kusini na kati yao ni mmoja tu ndiye anayejua lugha ya kiingereza.

Akiongea na waandishi wa habari Afisa uhamiaji wa mkoa wa Mtwara James Mwanjotile amesema watu hao 67 kati yao ni 14 tu wenye vibali vya kusafiria yaani passport lakini hawakupita katika vituo vya uhamiaji kwa ajili ya kufuata taratibu za kusafiri.

Aidha wahamiaji wengine 7 wamekamatwa wilayani Tandahima na kufanya jumla ya wahamiaji kufikia 74 ambao tayariwamefikishwa mahakamani kwa kosa la kuingia nchini bila kufuata taratibu.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.