Mgodi wa ACACIA umesaini mkataba na Halmashauri ya Msalala na Nyangh’wale kuanza mradi mkubwa wa maji kutoka Ziwa Victoria utakaogharimu shilingi bilioni 4.5 na kunufaisha vijiji 14.
Wakizungumza katika Siku ya Familia iliyoandaliwa na Mgodi huo Mkuu wa Wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu amesema tatizo la Maji ni Changamoto ya nchi nzima na mradi huu utasaidia kwa kiasi kikubwa.
Mradi huo unasimamiwa na Mwauwasa utawanufaisha wakazi laki na nusu
Miradi ambayo Mgodi iliahidi kufanya kabla ya kupunguza uzalishaji itaendelea kama kawaida.
Miradi mingine mikubwa inayotekelezwa na Acacia baadhi yake ni ujenzi wa majengo awamu ya pili kukamilisha Hospitali ya Bugarama uliogharimu bilioni 1.1 na milioni 200 zimetumika kujenga uzio katika Shule ya Msingi Kakola A na B.
Picha na mtandao.