Star Tv

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu miaka 30 jela watu watano akiwemo Mfanyabiashara Moriss Malianga maarufu kama ‘Rais wa Sinza’ baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la unya’nganyi wa kutumia silaha.

Wengine waliohukumiwa ni pamoja na Flano Masulu (Singu), Jeremiah Mgori, Sandru Kamugisha na Sadick Bwanga. Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri ambapo amesema mahakama imeridhika na ushahidi wa upande wa mashtaka ambao umethibitisha mashtaka dhidi yao.

Awali katika kesi hiyo namba 14 ya mwaka 2016, wakili wa utetezi Nehemiah Nkoko aliomba wateja wake wapatiwe nafuu ya adhabu. Katika kesi hiyo, washtakiwa wanadaiwa December 22, 2015 maeneo ya Mabibo Luhanga washtakiwa waliiba Dola za Marekani 8,600 ambayo ni sawa na Sh.Mil 18 kwa wakati huo.

Pia wanadaiwa waliiba tena Tsh milioni 2.5,  laptop moja na simu nne vyote vikiwa ni mali za Anderson Balongo na baada ya kuiba walimtishia kwa bastola Zeno Mriwa, Aneth Paulo, John Mkundi ili kujipatia mali hizo.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.