Star Tv

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa bado hawajakabidhiwa nyaraka walizoziomba kutoka kwa aliyekuwa Rais wa klabu ya Simba.

Evans Aveva anayekabiliwa na kesi ya utakatishaji fedha wa USD 300,000 ili wapate nyaraka za upelelezi.

Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa TAKUKURU, Leonard Swai amemueleza Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa kuwa kesi ilipangwa kwa ajili ya kutajwa, pia upelelezi bado haujakamilika.

Pia Swai amedai kuwa bado hawajakabidhiwa nyaraka walizoziomba kutoka Ofisi ya Aveva ili wakamilishe upelelezi.

Hata hivyo, upande wa utetezi umeieleza mahakama kuwa wameipokea barua ya TAKUKURU kuhusu maombi hayo na wanayafanyia kazi.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Nongwa ameahirisha kesi hiyo hadi January 11,2018.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.