Star Tv

Serikali imezielekeza Halmashauri zote nchini kuanisha maeneo ya kimkakati ili ujenzi wa vituo vya afya vijengwe katika maeneo hayo na kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya Dkt. Festo Dugange wakati akijibu maswali bungeni leo kwa niaba ya Waziri wa Nchi wa Ofisi ya Raia TAMISEMI wakati akijibu swali la Mbunge wa Magu Kiswaga aliyetaka kujua lini Serikali itapeleka huduma ya vituo vya afya katika vijiji vya Lutale, Kwamanga na Igogo.

Dugange ameongeza kuwa Serikali ilishatoa utaratibu na kuzielekeza Halmashauri zote nchini kuanisha Kata za kimkakati kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya.

Ameongezea kuwa ujenzi wa vituo vya afya utazingatia vigezo na si kila eneo litajengwa vituo hivyo.

Aidha, ametoa wito kwa Mbunge na Mkurugenzi wa Halamshauri ya Wilaya Magu kushirikiana na Ofisi ya Rais – TAMISEMI kuangalia na kuanisha maeneo yenye vigezo hivyo ili hatua za haraka zichukuliwe ujenzi uanze na wananchi wapate huduma.

Mapema Naibu Waziri amewatoa hofu Waheshimiwa Wabunge kuwa, ujenzi wa vituo vya afya vitakavyojengwa ni pamoja na ununuzi wa vifaa tiba amesema, bajeti ya mwaka 2022/23 Serikali imetenga sh. bilioni 69.95 ambapo vifaa hivyo vitaenda kwenye vituo vya afya 530 vinavyojengwa nchi nzima.

“Ninapokea shukrani za Mbunge wa Rungwe Antony Mwantona kwa kazi kubwa iliyofanywa na Serikali kwa kujenga vituo vya afya vitatu ndani ya mwaka mmoja ndato, kimwa, imenjora” - Dugange

Aidha ameongeza kuwa, vituo vya afya vilivyokamilika vitapewa kipaumbele kwa kupatiwa vifaa tiba ili viweze kutoa huduma na wananchi waweze kupata huduma.

Dugange amesema, Serikali itaendelea kusimamia sekta ya afya na kuendelea kuweka mipango mizuri ili vituo vyote vinavyojengwa kuwekewa vifaatiba.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.