Star Tv

Pembejeo feki za kilimo zimetajwa kuharibu mpango wa serikali wa uanzishwaji wa Viwanda nchini, huku zikidaiwa kudumaza hali ya uchumi wa wakulima kwa kushindwa kupata mavuno yale waliyokusudia na hivyo kujikuta wakiendesha kilimo kisicho na tija.

Ni msimu wa kilimo ambapo wakulima katika mikoa mbalimbali nchini wapo mashambani kutimiza wajibu wao, huku changamoto ya uuzaji wa pembejeo feki inayofanywa na baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu kwa kusambaza na kuuza mbegu zisizofaa inadaiwa kukinzana na matamanio ya serikali ya awamu ya tano inayohimiza viwanda ambavyo malighafi zake nyingi zinategemea mavuno yatokanayo na kilimo

Changamoto nyingine zilizotajwa na wakulima kuwa ni kuchelewa kwa pembejeo za ruzuku.

Umoja wa wafanyabiashara wa pembejeo za kilimo mkoa wa Njombe, kupitia katibu wake Waziri Kindamba amesema suala la uuzaji wa pembejeo feki wanalikabili ipasavyo na kuwa wao kama wafanyabiashara changamoto kuu ni namna ya kuwafikia wakulima wa pembezoni na bei elekezi.

Picha na mtandao.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.