Star Tv

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Ummy Mwalimu ameagiza viongozi wawili kukamatwa na kusimamishwa kazi kwa kwenda kinyume na maagizo ya serikali.

Viongozi hao wawili ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyamlilio na mtendaji wa kijiji hicho wilayani Sengerema Mkoani Mwanza, ambao wamekutwa na madai ya kuwachangisha wananchi kwa nguvu fedha za maendeleo na ikiwa wanashindwa kutoa michangi viongozi hao hukamata mifugo yao.

Aidha, kufuatia malalamiko hayo, Waziri Ummy ameagiza watendaji wote wa vijiji na kata nchi nzima wasichangishe fedha kwa wananchi bila kibali kutoka kwa mkuu wa wilaya husika.

Mkazi wa Kijiji cha Nyamililo, Sijali Matihas amedai kuwa Machi 18 mwaka huu, mtendaji na mwenyekiti huyo walifika nyumbani kwake wakachukua mbuzi jike; "baada ya siku tano nilikwenda ofisi ya mtendaji na Sh30,000 kwa ajili ya kuchukua mbuzi wangu lakini kitendo kilichofanyika pale nilikosa amani"-Alibainisha Mathias.

Kwa upande wake mtendaji wa kijiji hicho Mariamu Mugunda amesema michango hiyo walikubalina na wananchi kupitia vikao vyote vya kijiji hicho na hajaenda kinyume na utaratibu.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.