Star Tv

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza SACP. Ramadhani Ngh'anzi amethibisha kuwakamata viongozi 15 wa CHADEMA akiwemo Mwenyekiti wa chama hicho taifa Freeman Mbowe.

 Kamanda Ngh'anzi amesema Mwenyekiti huyo wa CHADEMA yupo Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano kufuatia kuwa na tuhuma nyingine katika mkoa huo.

"Baada ya kumkamata, wenzetu wa Dar es Salaam nao walitueleza kuwa wanamtafuta kwa makosa mengine anayodaiwa kuyafanya huko, hivyo tulimsafirisha kwenda Dar es Salaam anakoendelea kuhojiwa," - Amesema Kamanda Ng'anzi.

Aidha, Kamanda Ng'anzi amefafanua kuwa mara baada ya mahojiano yake na Jeshi la Polisi mkoani Dar es Salaam, atarejeshwa Mwanza ili aungane na wenzake wanaoshikiliwa kuhusiano na Kongamano la Katiba mpya ambalo hapo jana lilizuiliwa kufanyika.

Kamanda Ngh'anzi, amefafanua kuwa Mbowe alitiwa mbaroni alfajiri ya kuamkia jana Jumatano Julai 21 akiwa hoteli ya Kingdom mkoani humo, na kwamba viongozi wengine wa chama hicho wanaendelea kushikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Mwanza.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.