Star Tv

Uelewa mdogo wa kina juu ya Elimu ya Ukimwi kati ya watu wazima na Vijana na Kuanza mahusiano ya Ngono katika umri mdogo kunatajwa kuwa ni sababu zinazochangia maambukizi Mapya kuwa makubwa kwa vijana Tanzania.

Hayo yamebainika katika warsha ya Wabunge wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Ukimwi na tume ya kudhibi Ukimwi TACAIDS mjini Dodoma Mkurugenzi wa ufatiliaji wa Tathimini kutoka Tume hiyo Dr. Jerome Kamwela akabainisha hali ilivyo kwa sasa hapa nchini.

Mkurugenzi wa Tume hiyo Dr. Leonard Maboko akatolea ufanunuzi suala la mkanganyiko wa Takwimu Baadhi ya wajumbe wa kamati ya Bunge ya Ukimwi wakatoa mtazamo wao kuhusiana na juhudi zinazofanyika katika mapambano dhidi ya Ukimwi Waziri wan chi ofisi ya waziri mkuu Jenister Mhagama akawataka wajumbe kutumia vyema elimu watakayoipata.

Aidha Kiwango kidogo cha upimaji wa VVU kwa watoto waliozaliwa na akina mama wanaoishi na VVU Kunaelezwa kuwa ni moja kati ya changamoto katika kutekeleza Muitikio wa UKIMWI.

Picha na mtandao.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.