Uelewa mdogo wa kina juu ya Elimu ya Ukimwi kati ya watu wazima na Vijana na Kuanza mahusiano ya Ngono katika umri mdogo kunatajwa kuwa ni sababu zinazochangia maambukizi Mapya kuwa makubwa kwa vijana Tanzania.
Hayo yamebainika katika warsha ya Wabunge wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Ukimwi na tume ya kudhibi Ukimwi TACAIDS mjini Dodoma Mkurugenzi wa ufatiliaji wa Tathimini kutoka Tume hiyo Dr. Jerome Kamwela akabainisha hali ilivyo kwa sasa hapa nchini.
Mkurugenzi wa Tume hiyo Dr. Leonard Maboko akatolea ufanunuzi suala la mkanganyiko wa Takwimu Baadhi ya wajumbe wa kamati ya Bunge ya Ukimwi wakatoa mtazamo wao kuhusiana na juhudi zinazofanyika katika mapambano dhidi ya Ukimwi Waziri wan chi ofisi ya waziri mkuu Jenister Mhagama akawataka wajumbe kutumia vyema elimu watakayoipata.
Aidha Kiwango kidogo cha upimaji wa VVU kwa watoto waliozaliwa na akina mama wanaoishi na VVU Kunaelezwa kuwa ni moja kati ya changamoto katika kutekeleza Muitikio wa UKIMWI.
Picha na mtandao.