Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta John Magufuli amefanya mabadiliko katika Baraza la Mawaziri kwa kuongeza idadi ya Wizara, kuteua Mawaziri na Manaibu Waziri wapya na kuwahamisha Wizara baadhi ya Mawaziri na Naibu Mawaziri.
Katika mabadiliko hayo Rais Magufuli ameongeza idadi ya Wizara na Mawaziri wake kutoka 19 hadi 21, na Naibu Mawaziri kutoka 16 hadi 21.
Rais Magufuli ametangaza mabadiliko hayo Ikulu jijini Dar es Salaam akiwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
I. Waziri – George Mkuchika
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
I. Waziri - Selemani Jafo
II. Naibu Waziri - Joseph Kandege
III. Naibu Wazri – George Kakunda
Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira.
I. Waziri - January Makamba
II. Naibu Waziri - Kangi Lugola
Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu.
I. Waziri - Jenista Mhagama
II. Naibu Waziri - Anthony Mavunde (Kazi, Vijana na Ajira)
III. Naibu Waziri - Stella Ikupa (Walemavu)
Wizara ya Kilimo.
I. Waziri - Dkt. Charles Tizeba
II. Naibu Waziri - Dkt. Mary Mwanjelwa
Wizara ya Mifugo na Uvuvi.
I. Waziri - Luhaga Mpina
II. Naibu Waziri - Abdallah Ulega
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
I. Waziri - Prof. Makame Mbarawa
II. Naibu Waziri - Mhandisi Atashasta Nditiye
III. Naibu Waziri - Elias Kwandikwa
Wizara ya Fedha na Mipango.
I. Waziri - Dkt. Philip Mpango
II. Naibu Waziri - Dkt. Ashatu Kijaji
Wizara ya Nishati.
I. Waziri - Dkt. Medard Kalemani
II. Naibu Waziri - Subira Mgalu
Wizara ya Madini.
I. Waziri - Angellah Kairuki
II. Naibu Waziri - Stanslaus Nyongo
Wizara ya Katiba na Sheria.
I. Waziri - Prof. Palamagamba Kabudi.
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
I. Waziri - Dkt. Augustine Mahiga
II. Naibu Waziri - Dkt. Susan Kolimba
Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga (JKT).
I. Waziri - Dkt. Hussein Ali Mwinyi
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
I. Waziri - Mwigulu Nchemba
II. Naibu Waziri - Mhandisi Hamad Masauni
Wizara ya Maliasili na Utalii.
I. Waziri - Dkt. Hamisi Kigwangalla
II. Naibu Waziri - Josephat Hasunga
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
I. Waziri - William Lukuvi
II. Naibu Waziri - Angelina Mabula
Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.
I. Waziri - Charles Mwijage
II. Naibu Waziri - Mhandisi Stella Manyanya
Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi.
I. Waziri - Prof. Joyce Ndalichako
II. Naibu Waziri - William Ole Nasha
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.
I. Waziri - Ummy Mwalimu
II. Naibu Waziri - Dkt. Faustine Ndugulile Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
I. Waziri - Dkt. Harrison Mwakyembe
II. Naibu Waziri - Juliana Shonza
Wizara ya Maji na Umwagiliaji.
I. Waziri - Mhandisi Isack Kamwelwe
II. Naibu Waziri - Jumaa Aweso
Wakati huo huo, Rais Magufuli amemteua Bwana Stephen Kagaigai kuwa Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kabla ya Uteuzi huo Kagaigai alikuwa Kaimu Karani wa Baraza la Mawaziri. Bwana Stephen Kagaigai anachukua nafasi ya Dokta Thomas Kashilila ambaye atapangiwa kazi nyingine.
Wateule wote wataapisha Jumatatu tarehe 09 Oktoba, 2017 saa 3:30 Ikulu jijini Dar es Salaam.