Star Tv

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeuambia Muungano wa Jeshi linaloongozwa na Saudi Arabia nchini Yemen ni lazima kuruhusu misaada ya kibinadamu kupelekwa tena nchini humo.

Muungano huo wa jeshi umefunga njia zote za ardhini, anga na za maji tangu siku ya Jumatatu,kufuatia mashambulio ya makombora yaliyorushwa katika mji wa Riyadh na waasi wa Houthi walioko Yemen.

Baada ya mkutano wake wa ndani Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeagiza kuondolewa kwa vizuizi hivyo kwa kusema kwamba hali ya kibinadamu ni ya kutisha.

Mkuu wa shirika la misaada la Umoja wa Mataifa Mark Lowcock ameonya kutokea kwa kubwa la njaa, iwapo misaada haitapelekwa Yemen.

Hata hivyo Muungano huo wa Jeshi umedai kuwa vizuizi vinahitajika kuweza kuizuia Iran kuwapatia silaha waasi wa Ki-Houthi.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.