Star Tv

Jeshi la Korea Kaskazini limesema kwamba liko tayari kuingia katika eneo lisiloruhusiwa shughuli za kijeshi linalogawanya nchi hiyo na Korea Kusini ambapo Korea Kaskazini imetishia kutuma jeshi eneo salama la mpakani.

Tishio hilo linatokana na makundi yaliyoasi na kutorokea Korea Kusini yanayosambaza propaganda Korea Kaskazini.

Wikendi iliyoisha,Kim Yo-jong, dada wa kiongozi wa Korea kaskazini Kim Jong-un, alisema kwamba ataagiza jeshi kuelekea eneo hilo.

Na sasa hivi jeshi linasema liko tayari kubadilisha eneo hil kuwa ngome yao na kugusia kuwa liko macho.

Wasiwasi kati ya nchi hizo mbili umekuwa ukiongezeka kwa muda sasa kwasababu ya vipeperushi ambavyo vimekuwa vikisambaa katika mpaka wa maeneo hayo mawili ambavyo kawaida huwa vinatumwa kwa njia ya maputo.

Waziri wa ulinzi wa Korea Kusini Jumanne amejibu vitisho hivyo kwa kusema kuwa inashirikiana na Marekani kufuatilia kwa karibu hatua za kijeshi upande wa Korea Kaskazini.

Korea Kaskazini na Kusini zinagawanywa na eneo lisiloruhusiwa shughuli za kijeshi katika mpaka wake ambao umegawanya nchi hizo mbili tangu Vita ya Korea miaka ya 1950.

Jumanne, jeshi la Korea Kaskazini lilisema linafuatilia hatua inatakayochukuliwa na jeshi lake kwenda eneo hilo ambalo haliruhusiwi shughuli za kijeshi, huku Mkuu wa jeshi alisema liko katika hali ya tahadhari na tayari kutekeleza hatua yoyote itakayochukuliwa na serikali.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.