Star Tv

Rais wa Marekani Donald Trump, ametangaza kuweka zuio kwa raia wa nchi za Ulaya kuingia nchini Marekani ili kudhibiti kuenea kwa virusi vya corona.

Hayo yamejiri katika hotuba ya rais Trump kwa njia ya Televisheni siku ya Jumatano, ambapo amesema safari zote za kutoka Ulaya zitazuiwa kwa siku 30 zijazo.

Visa 1,135 tayari vimethibitishwa nchini Marekani huku watu 38 wakiripotiwa kupoteza maisha Hatua ambayo inatazamiwa kuanza   kutekeleza zuio la rais Trump kuanzia usiku wa siku ya Ijumaa''. 

Tump alizungumza saa kadhaa baada ya Italia ambayo ni nchi iliyoathirika zaidi baada ya China kwa kutangaza kuchukua hatua kali amesema Umoja wa Ulaya ''umeshindwa kuchukua hatua za tahadhari.

Amesema kuahirishwa kwa safari hizo pia kutahusu biashara na usafirishaji wa mizigo kutoka Ulaya kuingia Marekani.

Pia ametangaza kutoa mkopo wa mabilioni ya dola kwa wafanyabiashara wadogo, na kutaka bunge la Congress kupitisha nafuu ya kodi ili kukabiliana na athari za mlipuko wa corona kiuchumi.

Maafisa wamesema hatari ya maambukizi ilikuwa chini, lakini hali ilibadilika baada ya ongezeko la idadi ya visa vipya vya maambukizi vilivyothibitishwa mwanzoni mwa mwezi Machi.

Jitihada za kudhibiti zimeanza na tayari vikosi vimepelekwa kwenye mji wa New Rochelle, ulio kaskazini mwa New York, ambapo mlipuko huo unaaminika kuanzia huko.

Gavana wa jimbo la Washington amepiga marufuku mikusanyiko katika kaunti kadhaa, jimbo lililo Kaskazini Magharibi ni kiini cha maambukizi nchini Marekani, kukiwa na idadi ya vifo 24 kati ya 38 nchi nzima.

Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.