Star Tv

Mahakama ya Israel leo Machi 10, 2020 imekataa ombi la Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu la kutaka kufungua kesi ya rushwa dhidi yake anbayo imeahirishwa  hadi wiki ijayo.

Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa tena Machi 17,2020 ambapo kwasasa imekuja wakati Netanyahu na washirika wake wa wakijaribu kuunda serikali huku wakikabiliwa na upinzani mkali kufuatia uchaguzi mkuu uliofanyika wiki iliyopita.

Wabunge walioko upande wa Netanyahu ambaye ni Waziri Mkuu wa kwanza kushtakiwa akiwa madarakani, wameiambia mahakama hiyo ya wilaya mjini Jerusalem kwamba hawakupokea nyaraka zote za upande wa mwendesha mashtaka kuhusu kesi hiyo na wametaka wapewe muda wa siku 45.

Netanyahu anashtakiwa kwa tuhuma za udanganyifu, suala la rushwa na utumiaji mbaya wa madaraka pia akidaiwa kupokea zawadi kama takrima kinyume cha sheria ambapo kwa upande wake Waziri mkuu Netanyahu amekanusha madai hayo.

                          Mwisho.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.