Star Tv

Maafisa wa serikali ya China wamethibitisha kuongezeka kwa idadi ya watu wanaopoteza Maisha kutokana na homa inayosababishwa na virusi vya corona.

Mpaka sasa idadi ya watu waliokufa imefikia 425, wengi wa wahanga wakiwa katika mkoa wa Hubei, ilikoanzia.

Aidha, kulingana na maafisa wa serikali ya serikali ya China  wamesema hadi sasa watu 20,438 katika maeneo yote nchini wameambukizwa homa ya virusi vya Corona katika.

Maafisa hao wameripoti pia visa 3,235, vingi vikiwa katika mkoa ulioathirika zaidi wa Habei ambapo kati ya watu 425 waliofariki kutokana na homa ya virusi hivyo hatari, 414 ambao wanatoka  mkoa huo.

Viongozi wa China wamekiri kuwepo kwa mapungufu na changamoto katika juhudi za kuzuia kuenea zaidi kwa maradhi hayo.

Vyombo vya habari vya serikali nchini humo vimearifu kuwa hospitali mpya iliyojengwa kwa muda wa siku 10 tu imekamilika na imeanza kuwapokea wagonjwa.

Hospitali hiyo inavyo vitanda 1,000, na nyingine yenye vitanda 1,500 inatarajiwa kuwa tayari mnamo siku chache zijazo.

                                                                                     Mwisho.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.