Star Tv

Baraza la Senate la Marekani, linalodhibitiwa na Warepublican, limepinga jaribio la pili la chama cha Democratic kutaka nyaraka na ushahidi katika mchakato wa kumuondoa Rais Donald Trump madarakani.

Mchakato huo ambao ni  watatu katika historia ya Marekani, ambapo  maseneta wa Republican walipiga kura 53 dhidi ya 47 ya Wademocrat na kuzuia muswada kutoka kwa kiongozi wa Democratic Chuck Schumer, kutaka idara husika ya rekodi, iwasilishe ushahidi kuhusu shughuli za Trump na Ukraine.

Awali, baraza hilo lilipiga kura kwa njia hiyohiyo na kuzuia juhudi za Democratic kutaka nyaraka na rekodi kutoka ikulu ya Rais- White House kuhusiana na suala hilo.

Viongozi wa chama cha Democratic wamewashutumu wenzao wa Republic kwa kile ambacho wamekitaja kuwa udanganyifu katika mchakato huo.

 Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.