Star Tv

Rais wa Marekani, Donald Trump ametangaza kuweka vikwazo vipya vya kiuchumi dhidi ya Iran, ambapo amesema nchi hiyo haitolipiza kisasi kwa kufanya mashambulizi ya kijeshi.

Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumzia mashambulizi ya makombora katika kambi mbili za Marekani nchini Iraq, kwa kusema kuwa Marekani iko tayari kuendeleza amani, ingawa

ukweli ni kwamba ina jeshi kubwa na lenye vifaa imara.

Kwa mujibu wa Trump, amesema  Iran inaonekana inajaribu kupunguza mvutano kati ya nchi hizo mbili ambao ulizidishwa makali na mauaji ya jenerali wa Iran, Qassem Soleimani aliyeuawa na Marekani wiki iliyopita.

Katika hotuba yake iliyosubiriwa kwa hamu, hapo jana Trump amesema hakuna mwanajeshi yeyote wa Marekani aliyejeruhiwa au kuuawa katika mashabulizi hayo ya jana.

Kuhusu mkataba wa nyuklia wa Iran, Trump amezitaka nchi washirika zilizobaki katika makubaliano hayo kujiondoa kama ambavyo Marekani ilifanya mwaka 2018.

Aidha, serikali ya Uingereza imekataa ombi la Rais Donald Trump wa Marekani la kujiondoa katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na kusema makubaliano hayo yana umuhimu kwa London katika upande wa masuala ya kiusalama.

                                                                                                     Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.