Star Tv

Raia nchini Ufaransa na Ujerumani wanapiga kura leo katika siku ya mwisho ya uchaguzi wa Bunge la Ulaya ambapo vyama vinavyopinga Umoja wa Ulaya pamoja na uhamiaji vinatumai kutoa changamoto kubwa.

Mbali ya Ujerumani na Ufaransa, ambayo ni mataifa yenye nguvu barani Ulaya, nchi nyingine karibu 20 wanachama wa Umoja huo zinapiga kura leo, ambayo ni siku ya mwisho ya uchaguzi huo wa Bunge la Ulaya. Zaidi ya wapiga kura milioni 400 wanashiriki uchaguzi huo katika mataifa 28 na matokeo rasmi yanatarajiwa baadaye leo jioni. Nchini Ujerumani, maoni ya umma ya kabla ya uchaguzi yalivipa nafasi ya ushindi wa asilimia 28 vyama ndugu vya kihafidhina vya CDU na CSU. Wanasiasa kutoka vyama vikuu nchini Ujerumani walitumia siku za mwisho kabla ya uchaguzi kutoa onyo dhidi ya kukipigia kura chama cha siasa kali za mrengo wa kulia, AfD, kinachopinga wahamiaji na Umoja wa Ualya.

CHANZO: Idhaa ya Kiswahili DW.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.