Star Tv

Mkutano wa baraza kuu la Umoja wa Mataifa unaendelea mjini New York huku viongozi wa dunia wakitoa mwito juhudi za haraka zifanyike kushughulikia ukosefu wa upatikanaji wa chakula wakati hofu ikiongezeka juu ya mavuno mabaya mwaka ujao kutokana na vita nchini Ukraine.

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz amesema kuna dharura ya kutoa fedha kukabiliana na ukosefu wa upatikanaji wa chakula. Waziri mkuu wa Uhispania Pedro Sanchez amemkosoa rais wa Urusi Vladimir Putin kwa kuivamia Ukraine akisema hakuna amani kukiwa na njaa na haiwezekani kukabiliana na njaa bila amani. Rais wa Marekani Joe Biden atauhutubia mkutano huo hivi leo ambapo anatarajiwa kutangaza msaada mpya kwa Ukraine. Katika hotuba yake ya kwanza kwenye mkutano wa hadhara kuu ya Umoja wa Mataifa rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema nchi yake itafadhili usafirishaji wa ngano ya Ukraine kwenda Somalia inayokabiliwa na kitisho cha njaa.

CHANZO: DW SWAHILI

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.