Rais wa Marekani Joe Biden ametangaza janga hilo kuwa limekwisha nchini humo, Ambapo amebainisha kuwa "hata kama idadi ya Wamarekani ambao wamekufa kutokana na Covid inaendelea kuongezeka lakini janga hilo halipo nchini, ingawa bado tuna tatizo ila hali inaimarika kwa kasi".
Katika mahojiano na kipindi cha CBS cha 60 Minutes kilichopeperushwa Jumapili, Biden alisema kuwa Marekani bado inafanya "kazi nyingi" kudhibiti virusi. Ukigundua, hakuna mtu aliyevaa barakoa, "Kila mtu anaonekana kuwa katika hali nzuri ... Nadhani inabadilika."
Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) alisema wiki iliyopita kwamba mwisho wa janga hilo unaonekana, huku Takwimu zinaonyesha kuwa zaidi ya Wamarekani 400 kwa wastani wanafariki kutokana na virusi kila siku.
Lakini maafisa wa utawala waliambia vyombo vya habari vya Marekani Jumatatu kwamba maoni hayo hayaashiria mabadiliko ya sera na hakukuwa na mipango ya kuondoa dharura inayoendelea ya afya ya umma ya Covid-19.
Mnamo Agosti, maafisa wa Wamerekani waliongeza dharura ya afya ya umma, ambayo imekuwa tangu Januari 2020, hadi 13 Oktoba.
Aidha takwimu kutoka Chuo Kikuu cha Johns Hopkins zinaonyesha kuwa wastani wa siku saba wa vifo kwa sasa unasimama zaidi ya 400, na zaidi ya 3,000 wamekufa katika wiki iliyopita.
Maafisa wa afya ya umma wameelezea matumaini ya tahadhari katika wiki za hivi karibuni kwamba ulimwengu unaelekea kupona kwa janga, lakini wanaendelea kuwasihi watu kuwa waangalifu.