Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imekanusha kuhusika kwa namna yeyote katika tukio la kumdunga kisu mwandishi Salman Rushdie.
Msemaji wa wizara amewaambia waandishi wa habari kwamba Iran haioni kwamba hakuna mtu anayestahili kulaumiwa na kushutumiwa isipokuwa yeye na wafuasi wake.
Wakala wa Rushdie jana Jumapili alisema kwamba wakati mwandishi huyo anakabiliwa na majeraha ya kudungwa kisu hali yake inaendelea vizuri.
Mshambuliaji alimdunga kisu mara kadhaa Rushdie siku ya Jumapili alipokuwa karibu kutoa hotuba kuhusu uhuru wa kisanii katika Taasisi ya Chautauqua magharibi mwa jimbo la New York.
#ChanzoVOA