Mwanamageuzi mkongwe wa Urusi ambaye pia ni mshauri wa Rais Vladimir Putin amejiuzulu katika wadhfa wake.
Anatoly ni mmoja wa washauri wa Putin ambaye amejiuzulu kutoka jukumu lake kama mjumbe wa kimataifa na ni afisa mkuu zaidi kujiuzulu tangu kuanzishwa kwa uvamizi wa nchini Ukraine.
Ripoti za Urusi zimesema kwa sasa Chubais yuko Uturuki na mkewe.
Bwana Chubais alipewa kazi ya kuratibu malengo ya maendeleo endelevu ya Urusi kimataifa.
Baada ya vita kuanza alichapisha picha ya kiongozi wa upinzani aliyeuawa, katika kile kilichoonekana kama ishara mbaya.
Chanzo kimoja kililiambia shirika la habari la Tass kuwa ameondoka Urusi na pia kujiuzulu uwakilishi maalum wa Rais Putin. Pia hajatoa maoni yoyote kuhusu kujiuzulu kwake.
"Ndiyo, Chubais amejiuzulu kwa hiari yake mwenyewe. Lakini ikiwa ameondoka [Urusi] au amebaki, hilo ni jambo lake binafsi," - msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov alisema.