Balozi wa China nchini Marekani anasema kuwa China haitatuma silaha na risasi kusaidia vita vya Urusi nchini Ukraine na kwamba Beijing "itafanya kila kitu ili kupunguza mzozo".
Maoni ya Qin Gang yanakuja baada ya Rais wa Marekani Joe Biden kumuonya mwenzake wa China Xi Jinping siku ya Ijumaa kwamba kutakuwa na "matokeo" ikiwa Beijing itatoa msaada wa kijeshi kwa Moscow.
Beijing ilikanusha ripoti za wiki jana kwamba ilikuwa tayari kuipatia Moscow silaha kama "habari zisizofaa", lakini Uchina imekuwa ikisita kuikemea Urusi kwa uvamizi wake.
Akizungumza na shirika la utangazaji la Marekani CBS, Gang alilalamika kwamba kulaaniwa na nchi za Magharibi "hakusaidii" na kwamba "diplomasia nzuri" inahitajika.