Urusi imeiomba China usaidizi wa kijeshi pamja na ule wa kiuchumikulingana na ripoti katika magazeti ya Financial Times na lile la New York Times.
Moscow inaitaka Beijing kuwapatia silaha ili kutumia nchini Ukraine, gazeti la Financial Times limesema.
Huku likikataa kuwataja baadhi ya maafisa wa Marekani iliowanukuu, Gazeti la Financial Timesliliripoti kwamba Urusi imekuwa ikiomba China kuwapatia usaidizi wa silaha tangu uvamizi ulipoanza.
Hatahivyo maafisa hao hawakusema ni aina gani ya silaha ambazo Urusi inaziomba.
Ripoti hizo zimesema kuwa kuna ishara kwamba China inajiandaa kuisaidia Urusi.
Ripoti moja katika gazeti la New York Times ikiwanukuu maafisa wa Marekani inadai kwamba Urusi pia inaomba msaada wa kiuchumi ili kukabiliana na athari za vikwazo.