Star Tv

Maafisa wa ulinzi wa Ukraine wameonya kuwa Urusi inatayarisha vikosi vyake kufanya mashambulizi ya kila namna kwenye mji mkuu wa Kyiv.

Taarifa ya Jenerali wa jeshi la Ukraine ilisema kuwa vikosi vya Moscow vimeanza kukusanya rasilimali kwa ajili ya kushambulia mji huo, huku vifaru na vitengo vya askari wa miguu vikiwa vinasonga mbele kuelekea mji wa karibu wa Irpin kuweka msingi.

Taarifa hiyo iliongeza kuwa makamanda wa Urusi wamekuwa wakivipatia vikosi vyao mafuta yaliyosafirishwa kutoka Belarus kupitia eneo la kutengwa la Chernobyl.

Kwingineko, maafisa waliripoti kuwa jeshi la Urusi lilikuwa likielekeza nguvu zake katika kuzunguka miji ya mashariki ya Kharkiv, Chernihiv, Sumy na mji wa kusini wa Mykolayiv.

#ChanzoBBC

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.