Maafisa wa ulinzi wa Ukraine wameonya kuwa Urusi inatayarisha vikosi vyake kufanya mashambulizi ya kila namna kwenye mji mkuu wa Kyiv.
Taarifa ya Jenerali wa jeshi la Ukraine ilisema kuwa vikosi vya Moscow vimeanza kukusanya rasilimali kwa ajili ya kushambulia mji huo, huku vifaru na vitengo vya askari wa miguu vikiwa vinasonga mbele kuelekea mji wa karibu wa Irpin kuweka msingi.
Taarifa hiyo iliongeza kuwa makamanda wa Urusi wamekuwa wakivipatia vikosi vyao mafuta yaliyosafirishwa kutoka Belarus kupitia eneo la kutengwa la Chernobyl.
Kwingineko, maafisa waliripoti kuwa jeshi la Urusi lilikuwa likielekeza nguvu zake katika kuzunguka miji ya mashariki ya Kharkiv, Chernihiv, Sumy na mji wa kusini wa Mykolayiv.
#ChanzoBBC