Star Tv

Mawimbi ya Tsunami yaliyosababishwa na mlipuko mkubwa wa volkano chini ya maji yameikumba nchi ya Pasifiki ya Tonga.

Picha za mitandao ya kijamii zilionyesha maji yakipita kwa kasi eneo la kanisani na nyumba kadhaa, na walioshuhudia walisema majivu yalikuwa yakianguka kwenye mji mkuu, Nuku'alofa.

Tahadhari ya tsunami iliyotolewa iliwafanya wakazi kukimbilia maeneo ya miinuko

Mlipuko wa volcano ya Hunga Tonga-Hunga Haʻapai ulisikika Pasifiki ya Kusini, ikiripotiwa hadi New Zealand na Australia.

Mji mkuu wa Tonga uko kilomita 65 Kaskazini ya eneo lililokumwa na mlipuko wa volcano, kwenye kisiwa kikuu cha Tongatapu nchini humo.

 

Mabomba ya gesi, moshi na majivu yanayomiminika kutoka kwenye volcano yalifikia kilomita 20 angani, Huduma za Jiolojia za Tonga zilisema.

Wenyeji walisema mlipuko huo ulisikika kama ngurumo ya radi, ikifuatiwa na anga giza huku mawingu ya volkeno yakianza "kunyesha majivu na kokoto ndogo".

Maeneo mengi ya Tonga yanakabiliwa na uhaba wa umeme, huku huduma za simu na intaneti zikikatizwa, Kumaanisha mawasiliano yalikatizwa. Lakini video kwenye mitandao ya kijamii zilionyesha msongamano mkubwa wa magari huku watu wakijaribu kukimbilia maeneo ya juu kwa gari.

#ChanzoBBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.