Star Tv

Karibu theluthi mbili ya wapiga kura wa Uswizi wameunga mkono ndoa ya jinsia moja katika kura ya maoni.

Asilimia 64 waliunga mkono hatua hiyo, na kuifanya kuwa moja ya nchi za mwisho magharibi mwa Ulaya kuhalalisha ndoa za jinsia moja.

Wanaharakati wamepongeza kura hiyo kama hatua ya kihistoria kufikia haki za wapenzi wa jinsia nchini humo.

Kabla ya kura hiyo, makundi ya kidini na vyama vya kihafidhina vilipinga mpango huo vikisema unahujumu maadili ya familia.

Uswisi imeruhusu wenza wa jinsia moja kusajili uhusiano wao tangu 2007, lakini haki zingine zimedhibitiwa.

Hatua hiyo itawawezesha wapenzi wa jinsia moja kusaili watoto.

Inafanya Uswizi kuwa nchi ya 30 duniani kuhalalisha ndoa ya wapenzi wa jinsia moja.

Hatua hiyo itawawezesha wapenzi wa jinsia moja kusaili watoto na inafanya Uswizi kuwa nchi ya 30 duniani kuhalalisha ndoa ya wapenzi wa jinsia moja.

 

Waziri wa Haki Karin Keller-Sutter amesema ndoa ya kwanza ya jinsia moja itafanyika mwezi Julai mwaka ujao.

#ChanzoBBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.